Tuesday 5 December 2017

Kero za Walimu sasa kushughulikiwa




KERO ZA WALIMU KUSHUGHULIWA  SIHA
Kero mbalimbali za walimu katika Halmashauri ya Wilaya ya siha kuendelea kushughulikiwa kwa karibu zaidi ili kuongeza kiwango cha ufaulu kwa shule za msingi na Sekondari.

Kauli hiyo imetolewa na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Siha Valerian Juwal mapema leo tarehe 4 desemba 2017 katika ukumbi wa mikutano wa RC Sanya Juu alipokutana na walimu wa shule za msingi kwa lengo la kufanya tathmini ya matokeo ya darasa la saba mwaka 2017.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Siha aliwataka walimu Wilaya ya Siha kufanya kazi kwa bidii na maarifa huku wakizingatia maadili ya kazi ya ualimu kwani taifa na jamii linawategemea walimu.

Alitoa wito kwa walimu wote wenye kero mbalimbali zinazowasumbua kufika ofisi ya mkurugenzi wakati wowote kwani ofisi yake ipo tayari kupokea na kutafutia ufumbuzi kero mbalimbali za walimu Wilaya Siha.

Hata hivyo,alieleza kuwa yapo matatizo na kero za walimu ambazo ofisi yake imekwisha zitatua mara baada ya kuzipokea kero hizo, naomba kutoa wito kwa walimu kutumia hata namba yangu ya simu kunipigia pale wanapoona kuwa hawapati huduma stahiki katika ofisi wanazofanyia kazi alisema Juwal.

Katika Tathmini hiyo ya matokeo ya darasa la saba kwa shule za msingi Siha mwaka 2017 shule zilizofanya vizuri ni pamoja na PUNCMI,SAMAKI,NGARONY,NKYARE,GARARAGUA,KYENGIA,FUKA ENG MED, LOKIRI NA FUKA.


No comments:

Post a Comment