Thursday 9 November 2017

DC SIHA kuwachongea Madiwani Kwa Wananchi




 Viongozi katika Wilaya ya Siha watakiwa kushiriki katika shughuli za maendeleo kikamilifu kwa lengo la kuwapatia Wananchi maendeleo ya kweli Chini ya Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na mhe. John Pombe Magufuli.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa Wilaya ya Siha mhe. Onesmo Buswelu mapema tarehe 8.11.2017 alipokuwa akikagua ujenzi wa wodi ya wazazi inayoendelea kujengwa hospitalini hapo Kwa michango ya Wananchi wa Wilaya ya Siha pamoja na wadau wengine wa maendeleo.

Alieleza kuwa wapo baadhi ya viongozi ambao bado hawajatoa michango yao hadi Sasa jambo ambapo linashangaza kuwa hawataki shughuli za maendeleo kufanikiwa au wana agenda yao binafsi aliuliza Buswelu.

Alisema kuwa wakati ukifika Kazi yake ni moja tu atawachongea Kwa wapiga Kura wao ili wawatambue kuwa viongozi waliowachagua hawataki maendeleo.

Mimi kama mkuu a Wilaya ya Siha napenda kuwakumbusha tena viongozi wenzangu tusiwaache Wananchi wenyewe katika suala la maendeleo kwani maendeleo ya kweli hayana itikadi za vyama wala ukabila wa Imani zetu za dini.

Aidha ,alieleza kuwa hata kama baadhi ya watu wenye nia mbaya na Siha hawatachangia na kushiriki katika uhamasishaji shughuli za maendeleo,Kazi  zitakwenda tu kwani wanaopinga maendeleo siku zote ni watu wachache.


Buswelu alitoa wito Kwa viongozi wa kuchaguliwa Wilaya Siha  kuendelea na Kazi ya kuwatumia Wananchi na kutimiza ahadi walizotoa wakati wakiomba Kura Kwa wananchi kama anavyofanya mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.



No comments:

Post a Comment