Utoaji wa Chanjo Wafanikiwa
Wilaya ya Siha mwaka 2016/2017
Halmashauri ya Wilaya ya Siha Mkoa wa Kilimanjaro imefikia
zaidi ya asimia 96 ya huduma ya utoaji
wa chanjo mbalimbali ya kujikinga na magonjwa kwa watoto Wilayani hapa.
Katika taarifa ya mwaka 2016/2017 iliyotolewa na Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya
Siha Valerian Juwal katika mkutano wa kawaida wa Baraza la Madiwani
lililokutana mwezi Oktoba katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha.
Taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji ilieleza kuwa katika huduma ya
utoaji wa chanjo mbalimbali kwa watoto, halmashauri ya Wilaya ya Siha
imefanikiwa kutoa chanjo ya matone ya vitamin A na dawa za minyoo hadi kufikia
asilimia 96.7
Aidha taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji ilieleza kuwa,katika
huduma ya utoaji wa chanjo ya kansa ya shingo ya kizazi kwa watoto wa kike
wenye umri chini ya miaka 14,zoezi hilo
pia lilifanikiwa kwa zaidi ya asilimia 87.
Mkurugenzi Mtendaji alieleza Baraza la Madiwani kuwa, Halmashauri ya Wilaya
ya Siha ni miongoni mwa Halmashauri za
Wilaya hapa nchini zilizofanya vizuri katika usimamiaji wa zoezi zima la utoaji
chanjo kwa watoto.
Alieleza kuwa siri ya mafanikio ya zoezi hilo ni ushirikiana wa dhati baina ya Wananchi ,viongozi na wadau wengine
wa maendeleo katika Wilaya ya Siha.
Hata hivyo, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Siha
aliwaomba wananchi na viongozi wa Siha kuendelea kuunga mkono jitihada za
serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania za kuboresha afya ya wananchi wake
hasa utoaji wa chanjo unaosaidia kutoa kinga mbalimbali kwa watoto.
Vile vile,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Siha alieleza
Baraza la Madiwani kuwa huduma ya chanjo zote alizozitaja hutolewa bure kwa
kugharamiwa na Serikali na hivyo kuwataka wananchi kutoa taarifa mara moja
iwapo watatokea watu wanaowadai fedha za kulipia huduma hiyo.
Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi iliyofanyika mwaka 2012
Halmashauri ya Wilaya ya Siha inajumla ya watu 116,313 wakiwemo wanaume 56,500
na wanawake 59,813.
No comments:
Post a Comment