Tuesday 1 August 2017

Jukwaa la Wanawake yazinduliwa rasmi Siha



Jukwaa la Wanawake yazinduliwa rasmi Siha
Wilaya ya siha mkoa wa Kilimanjaro limefanikiwa kuzindua jukwa la wanawake kufuatia agizo la serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kuwa kila wilaya kuwa na jukwaa hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Siha mhe Onesmo Buswelu amezindua jukwa hilo rasmi leo tarehe 01 Agosti 2017 ambapo uzinduzi huo umefantika katika ukumbi wa Kanisa Katoliki uliopo katika Kata ya Sanya Juu.

Katika hotuba aliyoitoa kwa wanawake wa Wilaya ya Siha,mhe Onesmo Buswelu ambaye pia alikuwa mgeni rasmi wa shughuli hiyo aliwataka wanawake kujiamini na kuchangamkia fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali ya Tanzania katika kujiletea maendeleo ndani ya jamii.

Alieleza kuwa Serikali inatambua kuwa mwanamke akipata elimu jamii itakuwa imeelimika kwa ujumla,hivyo wanawake wachangamke katika kujiunga na vikundi mbalimbali ili waweze kupatiwa mikopo na elimu ya ujasilia mali na ukuzaji wa uchumi.

Aidha,mkuu huyo wa Wilaya ya Siha aliwaambia wanawake kuwa Halmashauri ya Siha inatenga bajeti ya asilimia 5 ya mapato ya ndani kwa ajili ya mikopo ya wanawake na asilimia 5 ya mikopo kwa vijana  kila mwaka wa fedha.

Katika uzinduzi huo wa jukwaa la Wanawake pia uongozi wa wilaya ulichaguliwa na viongozi waliochaguliwa walikuwa kama ifuatavyo:- Mwenyekiti wa jukwaa la wanawake alichaguliwa Christina P kavishe na Katibu wa Jukwaa la wanawake ni Aisha S.  Mwiru.

Baada ya uchaguzi huo, mwenyekiti wa jukwaa la wanawake wilaya ya Siha Christine Kavishe aliwashukuru kinamama wote waliomchagua na kuahidi kuwaunganisha wote bila kujali itikadi za vyama vya siasa na imani zao za madhehebu ya  dini.

No comments:

Post a Comment