Wednesday 12 April 2017

Wananchi wa Siha Wafanya kweli ujenzi wodi ya Wazazi

 Baadhi ya sehemu ya Wananchi wa Kata ya Sanya Juu Wilaya ya Siha wakishiriki katika kuchimba msingi utakaotumika katika ujenzi wa wodi ya Wazazi katika Hospital ya Wilaya ya Siha. Zaidi y Shilingi milioni 297 zitatumika katika ujenzi wa wodi ya Kinamama,Shilingi milioni 80 wodi ya watoto na milioni 511 zitatumika katika ujenzi wa jengo la upasuaji.Kukamilika kwa ujenzi huo kutasaidia kuwapunguzia wananchi wa Siha gharama za usafiri na matibabu ya kwenda hospital ya Mawenzi na KCMC mjini Moshi.

 Wananchi wa Kata ya Sanya Juu Wilayani Siha wakishiriki katika nguvu kazi za kuanza kwa ujenzi wa wodi ya Wazazi katika Hospital ya Wilaya ya Siha.tukio hili limefanyika hivi karibuni ambapo viongozi mbalimbali walishirikiana na Wananchi katika kazi za kujitolea
Wananchi wakiendele na kazi za kuandaa msingi wa ujenzi wa wodi ya Kinamama

No comments:

Post a Comment