Tuesday 4 April 2017

Picha za matukio ya jinsi Wananchi wa Wilaya ya Siha walivyoshiriki katika kuanza kwa ujenzi ya wodi ya Kinamama

 Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe.Onesmo Buswelu akishiriki ktk uchimbaji wa msingi kwa ajili ya ujenzi ya wodi ya kinamama.zoezi hilo limefanyika leo humans tarehe 4.4.2017  ktk hospital ya Wilaya ya Siha na Kuhudhuriwa na Wananchi wengi wa Kata ya Sanya Juu.
 Baadhi ya kinamama wakishiriki katika kazi za uchimbaji wa msingi kwa ajili ya ujenzi huo
 Mhe.Juma Jani Diwani wa Kata ya Sanya Juu akishiriki katika kazi ya ujenzi ya wodi hiyo mapema Leo jumanne tarehe 4.4.2017

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Siha Mhe.Frank Tarimo akishiriki vema katika kazi za uchimbaji wa msingi mapema Leo asbh katika eneo inapojengwa wodi ya Kinamama
 Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe.Onesmo Buswelu(aliyeshika kipaza sauti) akiwashukuru wananchi waliofika na kushiriki katika hatua za awali za kuchimba msingi wa wodi ya Kinamama iliyoanzwa kujengwa.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi ,Ujenzi na Mazingira Halmashauri ya Siha Mhe.Robert Mrisho akishiriki katika shughuli za kazi zilizokuwa zinendelea katika viwanja vya Hospital ya Wilaya ya Siha
 Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu ,Afya na Maji Mhe.Witson Nkini akimwagilia maji mti alioupanda karibu na eneo inapojengwa wodi ya Kinamama


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha  Valerian Juwal akishiriki katika kazi za mikono za kuchimba msingi kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya Kinamama.kazi hiyo imefanyika mapema leo jumanne tarehe 4.4.2017 katika eneo la Hospital ya Wilaya lililopo Kata ya Sanya Juu Wilayani Siha

No comments:

Post a Comment