Wananchi wa Kijiji cha Sanya hoyee Kata ya Sanya Juu wapongezwa kwa ujenzi wa madarasa mawili ya shule mpya ya msingi
katika kijiji cha Sanya Hoyee.
Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe. Onesmo
Buswelu alipofika eneo linapojengwa shule hiyo leo tarehe 19 Juni,2017 na
kukagua shughuli za ujenzi zinazoendelea.
Mkuu wa Wilaya ya Siha aliwapongeza viongozi wa Kata na Vijiji kwa
kazi nzuri aliyoiona hasa ujenzi wa madarasa na matundu ya choo cha wanafunzi,aliwataka
wananchi na Wadau mbalimbali wa maendeleo kuendelea kuunga mkono juhudi za
Jamii katika kujiletea maendeleo.
Katika ujenzi huo hadi Juni,2017 wananchi wameshachangia zaidi ya
shilingi milioni 5 ambazo zimetumika katika shughuli mbalimbali za ujenzi huo.
Hata hivyo mkuu huyo wa Wilaya ya Siha ametoa shilingi laki mbili
kama mchango wake wa kuunga mkono juhudi za wananchi za kujiletea maendeleo.
Hadi sasa ujenzi umefikia katika hatua ya umaliziaji wa kuweka
rangi,kuweka vioo pamoja na umaliziaji wa vyoo vya wanafunzi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa choo wa walimu.
Kukamilika kwa shule hiyo kutasaidia kupunguza msongamano wa
Wanafunzi katika shule za msingi Meral,Sanya Juu na Kilingi. Shule hiyo mpya ya
msingi inatarajiwa kuanza rasmi mwezi januari mwaka 2018.
No comments:
Post a Comment